KWANINI ILIKUWA BOCCO,ROBERTINHO AWEKA WAZI KILA KITU
Kocha Mkuu wa Simba Roberto Oliveira ‘Robertinho’ amesema kwa kiasi kikubwa benchi la ufundi pamoja na wachezaji wamefurahi kuingia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Robertinho amesema hayop jana mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika na kufanikiwa kutinga hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa kutoa sare ya bao 3-3 na Power Dynamos ya Zambia. Mbrazil huyo amesema mchezo wa kufuzu hatua ya makundi si rahisi na wamekutana na mpinzani ambaye kwenye dakika zote wametoka sare. “Champions League hakuna mechi nyepesi, mechi zote ni ngumu. Nimejiandaa wiki yote hii kwa mbinu mpya kwenye kipindi cha pili. Kama wachezaji wangu wanapokuwa wamechoka ninaamua kumtumia Bocco. “Nimecheza na washambuliaji wawili, Kibu na baleke lakini ninahitaji straika mmoja kweye boksi, Bocco ameweza na tumepata matokeo kwa hiyo kama mwalimu naweza kudiriki kusema mabadiliko yangu yamenisaidia. “Tulifunga viungo wa mpinzani wangu, walikuwa zero. Nilichokifanya ni kufunga ...